• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Mrejesho |
    • Lalamika |
Musoma Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Wasifu wa Kijamii na Kiuchumi wa Halmashauri
      • Viongozi wetu
        • Mayors
        • Municipal Directors
    • Dira na Dhamira
    • Maadili yetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu ya Sekondari
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Usimamizi na Ununuzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Uhifadhi Maliasili na Mazingira
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
          • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
            • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Maeneo ya Viwanda
    • Usafirishaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za maji
    • Maombi ya Huduma
    • Uthibi wa Mazingira
    • Uthibiti wa Misitu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili ya Madiwani
    • Ratiba ya vikao
  • Miradi
    • Miradi inayopendekezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mwongozo wa kushughulikia Malalamiko
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Wasifu wa Kijamii na Kiuchumi wa Halmashauri
    • Miongozo na Nyaraka
    • Sheria ndogo
    • Majarida
    • Council Budget
      • New menu item
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Makala

Miradi yenye thamani ya Bilioni 1.1 yazinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru

Imewekwa: August 28th, 2017

Miradi yenye thamani ya Bilioni 1.1 yazinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru

Mwenge wa Uhuru umefungua,kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika jumla ya miradi 7 ya maendeleo iliyogharimu jumla ya shilingi bilioni 1.1 katika Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.

Ziara ya Mwenge wa Uhuru 2017 ilifanyika katika Halmashauri ya Manispaa ya Musoma tarehe 27.08.2017 ukutokea katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Miradi ya maendeleo iliyotembelewa, kuzinduliwa, kufunguliwa na kuwekewa mawe ya msingi ilikuwa ni pamoja na ufunguzi wa wodi ya wazazi, Ufunguzi wa vyumba 4 vya madarasa katika shule ya msingi Mwisenge, Ufunguzi wa vyumba 4 vya madarasa na klabu ya Mazingira shule ya sekondari Nyasho.

Miradi mingine iliyotembelewa na kufunguliwa ni pamoja na Ufunguzi wa kiwanda cha kuzalisha maji ya Kunywa, Uzinduzi wa kituo cha damu salama, Kutembelea mradi wa ufugaji wa samaki pamoja na ufunguzi wa barabara ya FFU-Nyasho Cabin M 330.

Awali akisoma risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mkuu wa  Wilaya ya Musoma Dr. Vicent Naano alimweleza kiongozi wa mbio za Mwenge kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma imekuwa mstari wa mbele katika kutekeleza kauli mbiu ya Serikali ya viwanda kwa vitendo ambapo maeneo ya uwekezaji wa viwanda yametengwa ikiwa pamoja na kuanza ujenzi wa viwanda hivyo.

“Naomba nikuhakikishie kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma iko makini katika kutekeleza maagizo yote na sera zinazoelekeza katika uwajibikaji na ujenzi wa uchumi madhubuti wa wananchi wa Manispaa ya Musoma” alisema.

Dr. Vicent aliongeza kuwa katika kuongeza wigo wa ajira za vijana Manispaa ya musoma imetenga maeneo maalum kwa ajili ya biashara za vijana na akina mama katika eneo la SIDO lililopo kata ya Nyakato.

Akitoa ujumbe wa Mwenge kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2017 Amour Hamad Amour aliitaka Halmashauri ya Manispaa ya Musoma kuhakikisha inaweka mazingira Mazuri ya Biashara ili kuongeza mapato yake.

“Ni vyema sasa mkaanza kufikiri namna nzuri ya kuwawezesha machinga kufanya biashara zao vizuri ikiwa ni pamoja na kuwaboreshea mazingira ya kufanyika shughuli zao ili walipe kodi na serikali iongeze mapato” alisema.

Ndugu Amour alisisitiza kauli mbiu ya ujenzi wa viwanda pamoja na umuhimu wa kuongeza thamani katika bidhaa zinazozalishwa na wajasiliamali wadogo.

“Niwaombe sana wafanya biashara wote muda wa kuuza malighafi umepitwa na wakati na badala yake ni vyema sasa wafanya biashara wetu wakaanza kufikiria kuuza bidhaa zilizoongezwa thamani” alisisitiza.

Aidha, ndugu Amour aliwataka wadau wote wa maendeleo pamoja na wananchi kupiga vita rushwa, Malaria, dawa za kulevya pamoja na mimba za utotoni ambazo zimekuwa kikwazo kikubwa kwa watoto wengi wa kike katika kuendelea na masomo yao.

Mwenge wa Uhuru hukimbizwa kila mwaka nchi nzima lengo kubwa likiwa kuhamasisha jitihada zinazofanywa na serikali katika kuleta maendeleo na ustawi wa jamii pamoja na kujenga uzalendo miongoni mwa watanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • Terms of Reference for the provision of construction supervision consultancy services for urban infrastructure development in Musoma Municipality under the TACTIC Project March 06, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO October 03, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC MTAMBI AIPONGEZA MANISPAA YA MUSOMA KWA KUPATA HATI SAFI YA UKAGUZI

    June 02, 2025
  • Mvua iliyoambatana na upepo yasababisha maafa Manispaa ya Musoma

    March 24, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI

    November 05, 2024
  • Watumishi waaswa kuchapa kazi bila kujali uchache wao

    September 08, 2022
  • Tazama zote

Video

Hotuba ya aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara
Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sisi ni nani
  • Dira na Dhamira

Viunganishi Linganifu

  • IKULU
  • Tovuti ya Mikopo ya wajasiriamali
  • Public Service Management
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Musoma Municipal Council

    Sanduku la Posta: Box 194 Musoma

    Simu: 0282622560

    Simu ya Mkononi: +255754013734

    Barua pepe: info@musomamc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.