• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Mrejesho |
    • Lalamika |
Musoma Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Wasifu wa Kijamii na Kiuchumi wa Halmashauri
      • Viongozi wetu
        • Mayors
        • Municipal Directors
    • Dira na Dhamira
    • Maadili yetu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu ya Sekondari
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Miundombinu, Vijijini na Mijini
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Usimamizi na Ununuzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Uhifadhi Maliasili na Mazingira
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
          • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
            • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Maeneo ya Viwanda
    • Usafirishaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za maji
    • Maombi ya Huduma
    • Uthibi wa Mazingira
    • Uthibiti wa Misitu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Huduma za Uchumi
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili ya Madiwani
    • Ratiba ya vikao
  • Miradi
    • Miradi inayopendekezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mwongozo wa kushughulikia Malalamiko
    • Fomu
    • Mpango Mkakati
    • Wasifu wa Kijamii na Kiuchumi wa Halmashauri
    • Miongozo na Nyaraka
    • Sheria ndogo
    • Majarida
    • Council Budget
      • New menu item
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa umma
    • Hotuba
    • Makala

RC Atoa Mwelekeo wa Musoma Aitakayo

Imewekwa: June 14th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Kigoma Malima amelitaka baraza la Madiwani kutekeleza wajibu wake wa kuisimamia Halmashauri kwa kuweka mbele agenda ya maendeleo ili kufukia malengo.

Mhe. Malima ameyasema hayo alipokuwa akilihutubia baraza la Madiwani katika mkutano maalum wa kujadili hoja za ukaguzi uliofanyika jana katika ukumbi mkuu wa Manispaa ya Musoma.

Mhe. Malima amesisitiza kuwa Manispaa ya Musoma lazima ibadilike and kuongeza kuwa ili kufikia maendeleo lazima viongozi na wataalam wajiulize maswali magumu yatakayopelekea kupata suluhisho la changamoto zinazokabili ukuaji wa Manispaa.

Aidha, alitahadhalisha kuwa bila kubadilika Musoma itakuwa Mji wa mwisho miaka michache ijayo.

“Maendeleo yana kazi kubwa, hapa ni ‘capital city’, ninyi ni wajanja tuzungumze basi mambo ya maendeleo”. Alisema Mhe Malima.

Pamoja na kuibadili Musoma kwa mtizamo wa maendeleo aliwataka madiwani wasimame kwenye kilele cha ukweli na haki ili kusimamia kwa ufanisi shughuli zote za maendeleo katika Manispaa.

Kuhusu Uwajibikaji wa Mashirika ya Umma

Mhe. Malima aliweka wazi dhamira yake ya kuyasimamia mashirika na taasisi zote zilizo chini yake na kuzitaka kuzingatia misingi ya uwajibikaji na weledi.

Mhe. Malima aliitolea mfano Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira(MUWASA) ambayo haikuwa na utendaji wa kuridhisha hatua iliyopelekea kuvunjwa kwa bodi yake na kusimamishwa kwa baadhi ya watendaji.

“Simuombi mtu radhi kwa MUWASA kwa sababu ndilo shirika langu nyeti, nikiona uozo lazima niseme, kuna watu nimewashika kubaya” alisema na kuongeza “ Na mimi nawajua wapigaji, nimewashika pabaya, siombi msamaha kwa jambo lililo kwenda vibaya”. Alisema Mhe. Malima.

“Kuna wabaya wanapeleka maneno kuwa yule jamaa anaondoka muda wowote, waambieni wanapoteza muda. Kila mtu abebe mzigo wake”.Alisisitiza Mhe. Malima.

Mhe. Malima alimtaka  kila anayehusika kuhakikisha anasimamia eneo lake na kuondoa dosari zote za kiutendaji zinazoweza kuleta maswali yasiyo na majibu kwa wananchi.

Uvuvi Haramu

Kuhusu uvuvi haramu Mhe. Malima alisema kuwa adui mkubwa  wa viwanda vya samaki ni uvuvi haramu na kuwataka wote wanaohusika kuacha mara moja vitendo hivyo.

Mhe. Malima aliongeza kuwa kiwanda cha ‘Prime Catch’ kilikuwa kinatoa ajira 700 lakini kutokana na uvuvi haramu samaki walipungua na hivyo uzalishaji wa kiwanda ulishuka hali  iliyopelekea kufungwa kwa kiwanda hicho na ajira kupotea.

“Ukimjua ndugu yako anafanya uvuvi haramu mwambie Mkuu wa Mkoa atabanana nae kila kona”. Alionya Mhe. Malima.

Upanuzi wa Uwanja wa ndege, eneo la Utawala na uwekezaji

Akizungumza kuhusu uwanja wa ndege Mhe. Malima lazima Manispaa ya Musoma iwe na uwanja wa ndege kwa maslahi mapana ya kiuchumi na  kuzihudumia kwa ufanisi rasilimali za hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Aliendelea kufafanua kuwa Musoma bila uwanja wa ndege haiwezi kupiga hatua kwa kuwa Musoma ndio pointi ya karibu kufika hifadhi ya Serengeti hivyo uwepo wa uwanja wa ndege utawavutia watalii wengi na fursa nyingine nyingi.

“Tunapozungumza kuhusu musoma lazima tujue tunalo tatizo kubwa.Musoma inazo rasilimali za pekee”. Alisema Mhe. Malima.

Mbali na rasilimali nyingi zilizoko Musoma wawekezaji wengi wamekuwa wakielekea mikoa ya jirani na mara nyingine kuhamisha biashara zao Musoma.

“Nataka wote tujiulize kwa nini watu hawawekezi Musoma?” aliuliza Mhe. Malima na kuongeza kuwa “Lipo tatizo na nawaambieni maneno magumu, makali, ili mjitafakari wenyewe, nyie ndio mliopewa dhamana na wananchi”.

Mhe. Malima alihitimisha hotuba yake kwa kulitaka baraza la Madiwani kuchukua hatua za makusudi kupanua eneo la Utawala la Manispaa kwa kufuata taratibu zote ili kuisaidia musoma kukua na kupata eneo la kupumulia.

“Lazima tukae kama madiwani tuchukue dhamana ya maendeleo ya mji wa Musoma. Nendeni mkaongee na jeshi na Halmashauri za jirani mpate maeneo ya viwanda na uwekezaji”. Alisema Mhe. Malima.

Awali akifunga mkutano wa Baraza la Madiwani Mstahiki Meya wa Manispaa ya Musoma Mhe. William Gumbo alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa  maelekezo na ushauri wake kwa maendeleo ya Manispaa ya Musoma na kuahidi kuchukua hatua kuanzia sasa ili kuibadilisha Musoma.  

Matangazo

  • Terms of Reference for the provision of construction supervision consultancy services for urban infrastructure development in Musoma Municipality under the TACTIC Project March 06, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MTENDAJI WA MTAA III October 05, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO October 03, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mvua iliyoambatana na upepo yasababisha maafa Manispaa ya Musoma

    March 24, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI

    November 05, 2024
  • Watumishi waaswa kuchapa kazi bila kujali uchache wao

    September 08, 2022
  • Dc musoma ataka ubunifu katika uanzishaji wa miradi ya kuongeza kipato

    September 08, 2022
  • Tazama zote

Video

Hotuba ya aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara
Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sisi ni nani
  • Dira na Dhamira

Viunganishi Linganifu

  • IKULU
  • Tovuti ya Mikopo ya wajasiriamali
  • Public Service Management
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Musoma Municipal Council

    Sanduku la Posta: Box 194 Musoma

    Simu: 0282622560

    Simu ya Mkononi: +255754013734

    Barua pepe: info@musomamc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.